Wednesday, February 29, 2012

OMMY DIMPOZ FT ALIKIBA - NAI NAI [www.DarTalk.com]

Jennifer Garner, Ben Affleck Welcome Baby Boy!

Already the parents of two beautiful daughters, Jennifer Garner and Ben Affleck are now the proud mom and dad of a beautiful baby boy as well! Congratulations!

The A-list couple, who got married back in 2005, have proven pretty skillfull at picking out pretty girl names, with Violet and Seraphina. The little boy's name?

Alas, mum's the word on the little guy's name for now.

Jennifer Garner, Ben Affleck

Jen and Ben with Violet, 6, last fall. Seraphina is 3.

"It would be so weird to have a boy," the actress told Ellen DeGeneres recently, but also said the experience would be absolutely "cool and different."

Affleck, in turn, said that the 3-against-1 female-to-male ratio in his house leaves him significantly outnumbered. Looks like he has a teammate at last!

"He knows when to swoop in with the gesture. He's sweet that way," the actress says of her husband. "Honestly, I would do anything for that man."

"I always know that it's not taken for granted."

Lordherry. Congrats again to the whole family!

Tuesday, February 28, 2012

MAKAMBA NA ZITTO UMRI WA KUGOMBEA URAIS UWE 35,



MBUNGE wa Bumbuli (CCM), January Makamba na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe wametaka umri wa kugombea urais wa Tanzania uanzie miaka 35 badala ya 41 kama ilivyo sasa.

Wakizungumza kwenye Kongamano la Katiba na Vijana lililoandaliwa na Taasisi ya Femina HIP, Dar es Salaam jana, Zitto na Makamba pia walitaka umri wa kupiga kura uanzie miaka 16 badala ya 18.

Akichangia hoja, Makamba alisema ili kugombea urais katika nchi nyingi za Afrika Mashariki, raia husika anatakiwa kuwa na umri wa miaka 35.

“Hatutakuwa tumeanza sisi kwa sababu nchi nyingi duniani nafasi ya urais inagombewa kuanzia miaka 35, kwa hiyo vijana tuangalie suala hilo katika mchakato wa Katiba Mpya inayokuja,” alisema.

Makamba alisema Katiba Mpya inayokuja iwawezeshe vijana kupiga kura wakiwa na umri wa miaka 16 badala ya 18: “Umri wa kuanzia miaka 16 unatosha kabisa kuchanganua ni kiongozi wa aina gani anafaa kuchaguliwa.”

Kauli ya Makamba iliungwa mkono na Zitto ambaye alizitaja nchi za Kenya, Uganda na Burundi kuwa urais unagombewa kuanzia miaka 35.

“Hata sisi Tanzania wagombea wetu wanaweza kugombea wakiwa na umri wa miaka 35 kama zilivyo nchi za wenzetu ili kuwapa vijana nafasi za kuongoza nchi,” alisema na kuongeza kuwa anamwunga mkono Makamba katika suala hilo.

Zitto akichangia hoja, pia aliunga mkono umri wa kupiga kura kuwa miaka 16 akisema hiyo itawapa nafasi vijana wengi kushiriki katika kuchagua viongozi wao.

“Zamani umri wa kupiga kura ulikuwa miaka 21, ukashushwa ikawa miaka 18, kwa wakati tulionao sasa, uwezo wa vijana ni mkubwa, wanaweza kuchagua viongozi wakiwa na miaka 16,” alisema.

Hata hivyo, Zitto alitoa angalizo kwa vijana akisema katiba pekee haiwezi kuwaletea maendeleo... “Vijana wasisubiri Katiba Mpya kuwa ndilo litakuwa suluhisho la matatizo bali, itaweka mazingira rafiki kwa vijana wanaojishughulisha.”

Aliwataka vijana wa Tanzania wasikwepe kujadili Katiba Mpya na kuwachia wanasiasa kwani jukumu hilo ni la kwao pia.

“Wanasiasa muda mwingi wanajadili mambo yanayohusu maslahi yao kama vile muda wa kukaa madarakani lakini, mambo yanayowahusu vijana yatajadiliwa kwa ufanisi na vijana wenyewe,” alisema Zitto.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Twaweza, Rakesh Rajani alisema vijana wanapaswa kuyapa kipaumbele masuala yanayohusu elimu kwa sababu huo ndiyo urithi usiohamishika.

“Elimu ndiyo kila kitu. Mnapojadili katiba angalieni mambo ambayo mnaweza kuyaweka katika Katiba Mpya,” alisema Rajani.

Meneja Uhusiano wa Femina HIP, Lilian Nsemwa alisema lengo la kuandaa kongamano hilo ni kuwawezesha vijana kutumia haki yao ya kushiriki katika mchakato wa kupata Katiba Mpya.

WAZIRI AMKANA DCI KANUMBA
















WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha amesema uchunguzi kuhusiana afya ya Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe bado unaendelea na ni yeye atakayetangaza matokeo ya kama alipewa sumu au la baada ya kukamilika huku akiikana ripoti iliyotolewa na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) Kamishna, Robert Manumba.

Hii ni mara ya kwanza kwa Nahodha kutoa tamko hilo tangu kuibuka kwa mjadala kuhusu afya ya Dk Mwakyembe hasa baada ya DCI Manumba kuutangazia umma kwamba ripoti kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inaonyesha kuwa Naibu Waziri huyo hakulishwa sumu, kauli ambayo ilipingwa na Waziri mwenye dhamana ya Afya, Dk Haji Mponda na Dk Mwakyembe mwenyewe.

Akizungumza katika mahojiano maalumu ofisini kwake Dar es Salaam jana, Nahodha alisema uchunguzi kuhusu afya ya Dk Mwakyembe ni wa kisayansi na hauwezi kufanyika ndani ya wiki mbili au mwezi.

“Ninachosema ni kwamba uchunguzi nilioutangaza bado unaendelea,” alisema na kuongeza: Sasa mimi nimetangaza matokeo ya uchunguzi? Mimi ndiyo Waziri nasema uchunguzi bado unaendelea na mimi ndiyo nitatangaza hitimisho la jambo hilo.”

Alisema suala la Dk Mwakyembe ni zito na siyo la mtu kukurupuka kwani linagusa hisia za watu na kutahadharisha baadhi ya watu wanaojaribu kulifanya jepesi wanachezea kitu hatari.

“Ndiyo maana nasema ni jambo linalohitaji weledi wa hali ya juu katika kulichunguza. Ni jambo zito la kisayansi, naomba nipewe muda ili uchunguzi nilioagiza ufanyike kwa kina. Nasisitiza ni jambo linalohitaji weledi wa kisayansi.”

Waziri Nahodha alisema uchunguzi huo unafanyika kwa kuhusisha jopo la wataalamu wa sayansi hivyo kuwataka Watanzania kutambua kwamba uchunguzi huo unaendelea na ni vigumu kutamka utakamilika lini.

Kuhusu ripoti ya DCI

Alipoulizwa ni kwa nini asimchukulie DCI Manumba hatua kwa kutoa tamko wakati uchunguzi alioagiza haujakamilika alisema: “Ndiyo maana nasema, uchunguzi wa suala hili unaendelea. Sasa hatima yote hayo unayozungumza nasema nipeni muda.”

Alipoulizwa ni wapi DCI Manumba alipata ripoti ya Dk Mwakyembe wakati mgonjwa mwenyewe na Waziri wa Afya wameikana, alijibu: “Sasa, hilo ni vyema ukamtafuta yeye mwenyewe DCI aseme. Mtafute aseme yeye na Waziri wa Afya, hao watu wawili wanaweza kuzungumzia ripoti hiyo, lakini mimi nasema uchunguzi wa jambo hili la Dk Mwakyembe ni wa kisayansi na bado unaendelea.”

Alisema alichokisema DCI Manumba kinaweza kuwa na msingi ambao anaujua mwenyewe hivyo, ni vyema akaulizwa yeye kuhusu undani wa ripoti yake huku akisisitiza: "Mimi ninavyoliangalia jambo hili la Dk Mwakyembe linahitaji umakini wa hali ya juu katika kulishughulikia. Hilo la DCI mtafute mwenyewe akueleze.”

Nahodha pia hakutaka kuzungumzia suala hilo kwa undani hata pale alipoulizwa ikiwa haoni kwamba kukanwa kwa kiwango hicho kikubwa kwa ripoti ya DCI Manumba kunawafanya wananchi waanze kutilia shaka utendaji kazi wa jeshi la polisi.

Hata hivyo, alipoulizwa jana kuhusu kukanwa kwa ripoti yake na mawaziri, akiwemo wa Mambo ya Ndani ambayo ndiyo wizara mama inayosimamia Jeshi la Polisi, DCI Manumba alisema kimsingi hawezi kujibizana na waziri yeyote kwani kufanya hivyo itakuwa ni utovu wa nidhamu katika utumishi wa umma.

Alisema alichokifanya ni kuandaa jalada ambalo tayari liko kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ambaye kwa mamlaka na utaalamu wake wa kisheria, ataamua cha kufanya baada ya kulipitia.

“Siwezi kujibizana na waziri wangu au waziri yeyote. Kama amesema uniulize mimi, ninachoweza kusema ni kwamba tayari nimeandaa jalada liko kwa DPP. Sasa nikianza kuzungumza hili au lile itakua haina maana watu watasema nimeanza kujitetea,” alisema.

DCI, Dk Mwakyembe na Dk Mponda

Akizungumza na waandishi wiki mbili zilizopita, DCI Manumba alisema: “Ukweli kuhusu kauli hiyo inayodai kuwekewa sumu, tumeupata baada ya kuwasiliana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ambayo nayo imewasiliana na hospitali aliyokuwa amelazwa Dk Mwakyembe nchini India. Taarifa zinaonyesha kuwa hakuna sumu.”

“Hatua zaidi zinachukuliwa dhidi ya jambo hilo, kwa sasa litashughulikiwa kwa kufuata misingi ya kisheria,” alisema Manumba.

Hata hivyo, siku moja baada ya kauli hiyo ya DCI Manumba, Dk Mwakyembe alitoa taarifa kwa vyombo vya habari akisema: "Napata tabu kuamini kama DCI Manumba na wenzake waliisoma taarifa halisi ya matibabu yangu au walisoma taarifa ‘nyingine’ na kama waliisoma taarifa hiyo wenyewe au ‘walisomewa!’

“Nasema hivyo kwa kuwa alichokisema DCI Manumba kwa waandishi wa habari, hakifanani kabisa na picha iliyoko kwenye taarifa halisi ya Hospitali ya Apollo inayotamka wazi kuwa kuna kitu kwenye bone marrow (uboho) kinachochochea hali niliyonayo, kitu ambacho mabingwa wanahangaikia kukijua, kukidhibiti au kukiondoa huku vyombo vyetu vya dola vikipelekeshwa na mafisadi kusema bila msingi wa kisayansi wala aibu: “Hakulishwa sumu”, “hakulishwa sumu.”

Dk Mwakyembe pia alitoa sababu kuu tatu za kupinga ripoti ya DCI Manumba: “Kwanza kwa kuingilia mchakato wa matibabu yangu na uchunguzi wa kina kuhusu kiini chake, unaoendelea katika Hospitali ya Apollo, India ambako bado sijahitimisha matibabu yangu, pili kwa ufinyu wa uelewa unaojitokeza bayana kwenye tamko la Jeshi la Polisi unaosisitiza kuwa ‘sikunyweshwa sumu’ wakati sumu si lazima unyweshwe ili ikudhuru, inaweza kudhuru hata kwa kugusishwa tu.

Tatu ni kitendo cha Polisi kujiingiza kwenye suala ambalo kwa takriban mwaka mzima sasa, halijawahi kuwa na dhamira ya dhati ya kulielewa au kulichunguza mbali na kulifanyia mzaha kupitia magazetini.

Januari 19, mwaka huu gazeti hili pia lilifanya mahojiano maalumu na Waziri Mponda ambaye naye alisema kwa utaratibu, ripoti ya daktari ni ya mgonjwa... “Sisi hatujaandika ripoti, muulizeni DCI Manumba awape ufafanuzi.”

Alisema wanaoweza kuzungumzia maradhi ya Dk Mwakyembe ni familia yake au yeye mwenyewe kwani ndiye mwenye ripoti. Lakini wizara haiwezi kufanya hivyo.

Thursday, February 23, 2012

MAUAJI SONGEA


MJI wa Songea na viunga vyake jana ulikumbwa na machafuko makubwa yaliyofanya polisi waue watu wanne baada ya wananchi kuandamana wakipinga mauaji yanayodaiwa kuambatana na imani za kishirikina tangu Novemba mwaka jana.

Katika machafuko hayo watu wengine 41 walijeruhiwa, wawili wakiwa katika hali mbaya huku shughuli za kiuchumi na kijamii zikisimama kwa muda.

Hata hivyo, idadi hiyo ya vifo na majeruhi inatofautiana kati ya ile iliyotolewa na jeshi la polisi, uongozi wa Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Wakati polisi ikisema waliokufa ni wawili na majeruhi ni 10, uongozi wa hospitali ya mkoa umesema umepokea maiti nne na majeruhi 41 na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa inasema waliokufa ni wawili na majeruhi ni 20.

Tukio hilo la kwanza kutokea katika historia ya Mji wa Songea, lilitokana na hatua ya wananchi kuamua kuandamana kuelekea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kuelezea kilio chao baada ya kuwepo kwa mauaji ya mara kwa mara ya raia tangu Novemba mwaka jana ambao baada ya kuuawa wamekuwa wakinyofolewa sehemu zao za siri.
Hadi jana, imeripotiwa kwamba watu tisa wameshapoteza maisha katika mazingira hayo kwa nyakati tofauti. Habari zilizopatikana mjini Songea zinasema kwamba mauaji hayo yanayohusishwa na imani za kishirikina yakidaiwa kufanywa na wachimba madini wa migodi iliyoko nchi jirani.
Maandamano na vurugu

Maandamano hayo yaliibuka baada ya jana asubuhi mtu mmoja wa kiume kukutwa amekufa kwa kukatwa mapanga eneo la Makarawe huku pia sehemu zake za siri zikiwa zimenyofolewa.

Baada ya kuuona mwili huo wa marehemu, umati wa watu ulianza kukusanyika na kuamua kuandamana wakisema kwa amani ili kuwasilisha kilio chao kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.

Maandamano hayo yalivuta umati watu na mamia ya wananchi walijiunga na kuanza kutembea kwa miguu huku wengine wakiwa katika pikipiki maarufu kwa jina la 'Yeboyebo,' kuelekea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa zilizo jirani na Makao Makuu ya Polisi Mkoa wa Ruvuma.

Kadri wananchi hao walivyokuwa wakiendelea kuandamana, habari zilitapakaa mitaa mbalimbali na kuwafanya wananchi wengi zaidi kuungana nao, hali iliyowalazimu polisi nao kujipanga kuwazuia kwa kutumia mabomu ya mchozi.

Hata hivyo, wananchi walizidi kuongezeka wakipinga hatua hiyo ya polisi kuwazuia kufikisha ujumbe wao kwa Mkuu wa Mkoa. Katika hatua hiyo, ndipo vurugu zilipoanza kwani wakati polisi watumia mabomu ya kutoa machozi, baadhi ya waandamanaji walianza kuvurumisha mawe hali iliyowafanya watu kukimbia huku na huko.

Vurugu zilishika kasi hali iliyowafanya polisi kuanza kutumia risasi za moto katika kile ilichodai baadaye kwamba ni katika kujilinda na ndipo vifo hivyo vilipotokea na idadi hiyo kubwa ya majeruhi. Hata hivyo, haikuelezwa mara moja kama miongoni mwa majeruhi hao alikuwamo askari polisi.

Baada ya mauaji hayo, vurugu zilizidi kusambaa katika mitaa mbalimbali ya Mji wa Songea huku wananchi wakianza kurusha mawe kuelekea Kituo Kikuu cha Polisi. Lakini wengine waliendelea kupigia kelele madai yao ya msingi huku wakilishutumu jeshi hilo kwa kushindwa kudhibiti mauaji hayo kwa muda mrefu.
Vurugu hizo zilisababisha ofisi za Serikali na taasisi binafsi mkoani Ruvuma kufungwa kwa muda yakiwemo maduka, masoko na huduma za kifedha katika mabenki kusimama kwa muda.

Huduma za usafiri katika stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani nazo zilisimama, huku madereva wa mabasi na abiria wakikimbia kujificha kuepuka mabomu ya machozi na risasi za moto zilizokuwa zikipigwa hewani.

Pia huduma za matibabu katika Hospitali ya Mkoa zilisimama kwa muda baada ya walinzi wa hospitali hiyo kufunga lango kuu, kutokana na wananchi wengi kukimbilia huko wakikimbia mabomu.

Habari zaidi kutoka eneo la tukio zimeeleza kuwa maandamano hayo yalichochewa na taarifa ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa juzi kwamba mauaji hayo yanahusiana na masuala ya kipenzi. Ilielezwa kwamba wananchi walikuja juu wakipinga madai hayo ambayo pia yaliripotiwa jana na gazeti hili.

Utetezi wa Polisi
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Michael Kamhanda alisema polisi ililazimika kutumia nguvu ya ziada baada ya wananchi kukaidi amri ya kuwataka watawanyike.
Alidai waliopoteza maisha kutokana na vurugu hizo ni wawili na majeruhi 10 akisema watu hao walifariki dunia kwa kupigwa risasi za moto baada ya kukaidi amri ya polisi kutawanyika.

“Tulilazimika kutumia risasi za moto baada ya hawa vijana kukataa kutii amri ya polisi,” alisisitiza Kamanda Kamhanda.
Kamanda Kamhanda alisema watu 56 wamekamatwa kwa ajili ya kuhojiwa kutokana na tukio hilo.
Kamanda Kamhanda alisema ingawa bado uchunguzi unaendelea, taarifa za awali zinaonyesha kuwa chanzo cha vurugu hizo ni imani za kishirikina na siasa. Hata hivyo, hakufafanua ushirikina wala siasa zilivyochochea maandamano hayo.
RC atoa amri ya kutombea usiku

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu alisema vurugu hizo zilizodumu kwa saa sita zimesababisha uharibifu mkubwa wa mali na kuhatarisha usalama katika mji huo.

Kutokana na hali hiyo, alitoa amri ya kutotembea usiku akisema msako wa kuwasaka watuhumiwa wa maandamano hayo bado unaendelea.

“Kama watakuwa hawana shughuli za muhimu wabakie tu majumbani mwao ili kuepuka usumbufu. Polisi itaendelea kuwasaka watuhumiwa usiku ili kuwabaini na kuwachukulia hatua za kisheria,” alisema.

Mkuu huyo wa Mkoa alitoa kauli hiyo baada ya kuongoza kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa kilichoitishwa ghafla kutokana na machafuko hayo makubwa.

Hospitalini
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma, Dk Benedicto Ngaiza alisema kati ya watu nne waliokufa na miili yao kupokewa, miwili ilikuwa na majeraha ya risasi na majeruhi wawili kati ya hao 41, walipelekwa chumba cha upasuaji kwa kuwa walikuwa na majeraha ya risasi pia.
“Hii miili ilikuja kwa awamu, mara ya kwanza ulikuja mmoja na mara ya pili ikaja mitatu. Yote ililetwa kwa magari ya polisi,” alisema Dk Ngaiza na kuongeza:
“Katika hii mitatu iliyokuja kwa pamoja miwili ilikuwa na majeraha ya risasi na mmoja alikuwa ni kijana aliyegonga mti na pikipiki akikimbia vurugu hizo. Kati ya majeruhi hao wawili wamepelekwa chumba cha upasuaji shida yao pia ni majeraha ya risasi.”

Kisa cha maandamano
Tangu Novemba mwaka jana, kumekuwa na matukio ya mauaji katika Mji wa Songea kwa nyakati tofauti hadi sasa ambayo yamekuwa yakitokea katika mazingira ya kutatanisha huku miili ya marehemu ikiwa imejeruhiwa kwa kukatwa mapanga, shoka au marungu na kunyofolewa sehemu za siri.

Hali imekuwa mbaya zaidi mwishoni mwa wiki ambako kwa siku tatu mfululizo mauaji hayo yalitokea hali iliyochochea hasira za wananchi hadi kufikia uamuzi wa kuandamana.

Watuhumiwa wanne wanaodaiwa kuhusika na mauaji hayo wanashikiliwa na polisi. Watuhumiwa ni Johari Kassim (16), Onesmo Hinju (14), Samason Haule (22) na Mussa Fuala (20) wote wakazi wa Mtaa wa Lizaboni mjini Songea.

Kilio chasikika

Kamati hiyo ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa imewataka watendaji na wenyeviti wa mitaa na mabalozi kuanzisha ulinzi wa doria za usiku katika maeneo yao kuanzia sasa na kwamba ambaye tukio la mauaji hayo ya kishirikina yatatokea katika mtaa wake atakamatwa na kuchukuliwa hatua.

Katika kikao cha kamati hiyo kilichowashirikisha pia viongozi hao, imeamuliwa pia kwamba watendaji hao wa ngazi ya msingi ya Serikali za Mtaa watalazimika pia kuwatambua wageni wote watakaofika katika maeneo yao ni pamoja na kuwataka waonyeshe vitambulisho vyao na wale watakaokuwa na shaka nao watoe taarifa zao katika vyombo vya sheria.