Tuesday, July 31, 2012

Zitto ahojiwa kwa rushwa

Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe
 
SAKATA la wabunge kuhusishwa na rushwa limeingia sura mpya, baada ya Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe kuhojiwa na chama chake cha Chadema kwa saa tatu jana.
Wakati Zitto akihojiwa, kambi rasmi ya upinzani bungeni, iliwataja wabunge saba wa CCM na kueleza kuwa ndiyo wanaolichafua Bunge kwa kujihusisha na mambo yenye maslahi binafsi wakiwa watumishi wa umma.

Kadhalika, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema kwamba Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (Takukuru) ilikuwa ikiendelea kuwahoji baadhi ya wabunge kuhusu tuhuma za rushwa na kwamba uchunguzi ukikamilika taarifa zitawekwa wazi.

Zitto ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, jana aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa Tweeter kwamba alihojiwa na Sekretarieti ya chama chake kutokana na tuhuma za rushwa zinazowagusa badhi ya wabunge.
Katika maelezo yake, Zitto alisema aliiambia sekretarieti ya chama hicho kwamba Chadema kifanye uchunguzi ili kubaini ukweli wa suala hilo na kwamba yuko tayari kuwajibika ikiwa itathibitika kwamba alihusika kula rushwa.

“Kwa saa tatu nimejieleza mbele ya sekretariati ya chama kuhusu tuhuma za rushwa dhidi yangu. Niliomba kutaka kutoa maelezo kwa Katibu Mkuu, nimekiomba chama kufanya uchunguzi na ikibainika hatua zichukuliwe,” inasomeka sehemu ya taarifa hiyo kwenye Tweeter.

Lissu ataja wengine
Kwa upande wake, Mnadhimu Mkuu wa kambi hiyo, Tundu Lissu aliwataja wabunge wa CCM ambao wanatuhumiwa kuwa ni Nasir Abdallah (Korogwe Mjini), Mariam Kisangi (Viti Maalumu), Vicky Kamata (Viti Maalumu) na Charles Mwijage (Muleba Kaskazini) ambao hata hivyo, wote wamekanusha madai hayo.

Wabunge wengine watatu tumeshindwa kuwataja kwa kuwa hawakupatikana kuzungumzia tuhuma dhidi yao.

Katika orodha hiyo wamo wawili wa Viti Maalumu na mmoja wa jimbo na Lissu alidai kwamba wamekuwa wakishiriki vikao vya Kamati ya Nishati na Madini huku wakijua kuwa wana maslahi binafsi na wengine kutumia fursa hiyo kujinufaisha.
“Kwa takriban juma moja sasa kumekuwa na mjadala mzito wa ufisadi hapa bungeni, sasa Kambi Rasmi ya Upinzani imejitathmini na kuona kwamba wabunge wake hasa walioko kwenye Kamati ya Nishati na Madini iliyovunjwa, John Mnyika, David Silinde na Mwanamrisho Abama hawahusiki,” alisema Lissu na kuendelea:

“Ila uchunguzi wetu umefanikiwa kupata majina ya wabunge wanaohusika moja kwa moja na mgongano wa kimaslahi ambao tunaona tuwataje kwa maslahi ya umma.”
Lissu alikwenda mbali zaidi na kutaja tuhuma zinazowahusu wabunge hao akisema wawili ambao gazeti hili halikuwaja, wamejihusisha kufanya biashara na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) hivyo wana mgongano wa kimaslahi.

Alisema Mwijage ana mgongano wa kimaslahi katika mchakato mzima wa kuipa zabuni ya kusambaza mafuta kampuni ya Puma Energy kwa kuwa yeye ni mtalaamu mwelekezi wa kampuni hiyo inayomilikiwa na Serikali kwa asilimia 50.
“Nasir Abdalah na Mariam Kisangi; Hawa wanamiliki vituo vya mafuta. Sasa kwa namna yeyote ile kuwa wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini hawawezi kutenda haki katika mchakato wowote unaohusu suala la mafuta,” alisema na kuendelea;

"....(jina limehifadhiwa) hana mgongano wa moja kwa moja wa maslahi, lakini kwa kadri tunavyofahamu, yeye ndiye aliyekuwa akiyafanyia kampeni ya kupata zabuni makampuni ya mafuta ya Oryx na Camel na ....(jina limehifadhiwa), suala lake ni complicated kidogo. Maslahi aliyonayo katika suala hilo ni kuwa ana uhusiano wa Kimapenzi na kigogo mmoja katika Wizara ya Nishati na Madini.”

“Hawa ndiyo wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini ambao sisi Kambi ya Upinzani tunawafahamu kuwa ndiyo waliojihusisha na mgongano wa kimaslahi. Tumewaangalia wabunge wetu wote watatu hawamo ila kama kuna mtu ana taarifa zinazowahusu, aseme na tutazifanyia kazi.”

Lissu alisema kitendo cha wabunge kujihusisha na mgongano wa kimaslahi na taasisi za umma ni kinyume na Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995 na ni kinyume na maadili ya kibunge.
Katika hatua nyingine Lissu amemshauri Spika wa Bunge Anne Makinda kuzivunja pia kamati za Bunge za Serikali za Mitaa (LAAC) na Kamati ya Mashirika ya Umma (POAC) akisema nazo zina madudu mengi.

“Hili lisiishie tu kwa kuvunja Kamati ya Nishati na Madini, tunataka pia kamati za POAC na LAAC zivunjwe, uchunguzi ufanyike na wahusika waitwe kujitetea na hatimaye wenye hatia watajwe hadharani bungeni na majina yao yachapishwe kwenye magazeti ili haki itendeke,” alisema.

Alipoulizwa Chadema imefanya nini dhidi ya Mbunge wake, Zitto Kabwe kutajwa katika orodha hiyo, alijibu: “Nikiri kwamba sisi taarifa tunazo ila hatujamwita kumwuliza. Naomba ieleweke kwamba kama chama au Kambi Rasmi ya Upinzani hatuna maslahi na mbunge yeyote anayeonekana kujihusisha na masuala hayo.”
“Katika hili tunaomba uchunguzi ufanyike na matokeo yake yatangazwe ili tupate msingi wa tuhuma hizo na ninaahidi kwamba tutazifanyia kazi ipasavyo.”

Majibu ya tuhuma
Alipotakiwa kuzungumzia tuhuma hizo, Kisangi alikiri kumiliki kituo cha mafuta lakini akasema sheria haimzuii mtu kama mambo yake anayafanya kwa uwazi.

“Nimekuja bungeni nikitokea kwenye ualimu, nilikuwa nafundisha Shule ya Msingi ya Mianzini na biashara hii ni ya familia. Inaendeshwa kwa uwazi na mwanangu wa kwanza ndiye anayeisimamia. Kutokana na uwazi katika shughuli zangu, mwaka jana Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma ilinipongeza. Mimi ni msafi na siko huko wanakofikiri wao (Chadema).”

Kwa upande wake, Mwijage alikanusha kuwa mtaalamu mwelekezi wa Kampuni ya Puma, badala yake akasema ni mtaalamu wa petroli anayefanya kazi ya kuishauri Serikali kuhusu mambo mbalimbali yanayohusu nishati hiyo.

"Siyo kweli, hawa wanadandia hoja. Mimi ni mtaalamu wa petroli ambaye mchango wangu kimsingi una faida kubwa bungeni na hata kwa jamii kwa ujumla. Sijafanya maamuzi yeyote ya kulihujumu taifa hili na hata kwenye Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini pekee, nilitoa mchango wa kurasa 10 kuhusu masuala hayo ya petroli,” alisema

Aliishauri kambi hiyo ya upinzani kuvuta subira, akieleza kuwa jambo lililoko bungeni linahusu ufisadi na uhujumu uchumi hivyo kauli zinazotolewa bila utafiti zinaweza kuvuruga mchakato mzima uliokwishaanzwa na Kamati ya Maadili ya Bunge.

Awali, Abdallah alipoulizwa kuhusu tuhuma za kumiliki vituo vya mafuta hivyo kuwa na maslahi binafsi, alicheka na kuahidi kwamba angepiga simu baadaye, lakini hakufanya hivyo na alipopigiwa baadaye alikata simu. Hata hivyo, alizungumza na waandishi wa habari na kukanusha kumiliki vituo vya mafuta.

Kamata kwa upande wake alisema: “Kuna kamati maalumu imepewa kazi ya kuchunguza mambo hayo, hivyo yote yanayoulizwa yatakuwa wazi na ukweli utajulikana tu. Nina maslahi au sina ukweli mtaujua, haraka ya nini?.

Mjadala Bungeni
Mjadala huo wa wabunge kuhusishwa na mgongano wa kimaslahi ulianza kulipuka bungeni jana asubuhi baada ya wabunge watatu; Joshua Nassari (Arumeru Mashariki), Salum Barwany (Lindi Mjini) na Mbunge wa Nkasi Kaskazni, Ali Kessy kutaka wabunge wanaotuhumiwa kwa ufisadi watajwe bungeni ili kuisafisha taasisi hiyo ya kutunga sheria.

"Mheshimiwa Naibu Spika juma lililopita Mheshimwa (Vita) Kawawa alitoa hoja kutaka suala la ufisadi lishughulikiwe kwa kuvunjwa Kamati ya Madini na Spika akaridhia na kulipeleka suala hilo kwenye Kamati ya Maadili. Kwa nini Kamati nyingine zilizohusishwa na ufisadi huo nazo zisivunjwe?” alihoji Nassari na kuendelea:

“Kuna Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) inayoongozwa na Mheshimiwa Mrema na Kamati ya Mashirika ya Umma (POAC) inayoongozwa na Zitto. Kuna tabia ya wabunge kuzikimbia kamati zisizokuwa na mikataba kama Kamati ya Huduma za Jamii na wanazikimbilia kamati zenye mikataba.”

Barwany alitaka Bunge litajiwe majina ya wabunge waliotuhumiwa kwenye kashfa hiyo mpaka wakapelekwa kwenye Kamati ya Maadili, akieleza kuwa hili litasaidia kulisafisha... “Tumeambiwa Kamati ya Maadili inajadili suala hilo, lakini hatujatajiwa ni wabunge gani waliopelekwa huko, tunaomba mtutajie ili Bunge lijisafishe.”

“Mimi naungana na wazo la Barwany na Nassari. Majina yatajwe wabunge tunadhalilishwa na wananchi huko mitaani. tuwataje hadharani,’ alisema Kessy.

Akitoa mwongozo wa hoja hiyo, Ndugai aliiagiza Kamati ya Uongozi ya Bunge kutoka kwenye ukumbi wa Bunge ili wakajadili suala hilo na baadaye apelekewe taarifa.
“Naamini wenyeviti wote wa kamati mmo humu ndani, naomba sasa hivi mwende kwenye Ukumbi wa Spika mkajadili suala hilo halafu nipate majibu sasa hivi,” alisema.

Baadaye jioni, Ndugai alisema kuwa Spika hawezi kuwataja kwa majina wabunge ambao wanajihusisha na rushwa kwa kuwa hawajui.

Alisema Kamati ya Uongozi iliyokutana jana mchana ilikubaliana kuwa ufanyike uchunguzi wa kina kwa ajili ya kuwabaini wale wanaoshukiwa na kwamba ikibainika Bunge litawaanika hadharani.

“Kamati imerejea kumbukumbu za hansard ya Jumamosi kuwa ufanyike uchunguzi wa kina juu ya jambo hilo na wabunge mtaitwa kwa ajili ya kutoa ushirikiano, ikumbukwe kuwa mbunge akiitwa siyo kwamba ndiyo amekuwa mtuhumiwa, bali pale itakapothibitika majina yatawekwa hadharani,’’ alisema Ndugai.
Naibu Spika alitahadharisha kuwa ndani ya Kamati hiyo utafanyika uchunguzi wa kutosha kubaini kama kuna mjumbe mwenye maslahi kwa wale wahusika basi ataondolewa ili kutoa nafasi kwa kamati kufanya kazi yake ipasavyo.

Aliwatahadharisha wabunge kuwa Kamati hiyo haitaingilia utaratibu wa vyombo vya dola ambao wamekuwa wakiufanya ikiwemo wa Takukuru wa kuwahoji baadhi ya wabunge.
 
source gazeti la mwananchi

Friday, July 27, 2012

FFU watoa wito kwa watanzania kuwapa shavu wanamichezo wetu !Olympic

Watanzana wameombwa kujitokeza kwa wingi katika kuwashingilia wanamichezo watanzania wanaoshiriki
katika michezo ya Olympic huko London, wito huo umetolewa na bendi maarufu ya Ngoma Africa aka FFU,
yenye makao yake Ujerumani.
Bendi ya Ngoma Africa inawaombea mafanikio na ushindi wanamichezo wa Tanzania,
Tuwaomba watanzana na marafiki wa Tanzania pamoja taha sisi mbali mbali zilizopo Uingereza na ughaibuni
kujitokeza kwa wingi na kuzipeperusha bendera za Tanzania kwa kuwashingilia wanamichezo wetu,kwa shangwe,
shangwe na mayoe ! Tanzania ! Tanzania! Tanzania! oyeeeeeeeeeee!
Mungu wabariki wanamichezo wetu! www.ngoma-africa.com

Mungu Ibaraiki Tanzania !

FFU Kuvuna walichopanda Ughaibuni!


Ngoma Africa band kupewa Tuzo la kimataifa,
 " IDA - International Diaspora Award"

Habari za uhakika zinatonya kuwa bendi maarufu ya muziki wa dansi
barani ulaya "The Ngoma Africa Band" au maarufu kwa jina la "FFU"
wazee wa virungu na makombora ya muziki,yenye makao yake
nchini Ujerumani, Bendi imetajwa kuwa ni bendi bora inayoitangaza miziki
ya Afrika kwa kasi duniani,na imechaguliwa kupewa tuzo maalumu la
" IDA - International Diaspora Award"  award , hiyo inatolewa na
tahasisi za kimataifa,itakabidhiwa kwa kiongozi wa bendi hiyo Kamanda
Ras Makunja wa FFU mwanzoni mwa mwezi wa nane.
Inasemekana Sherehe za kukabidhiwa TUZO hiyo zitafanyika mjini Tubingen,  
mkoa wa Baden württemberg, kusini mwa ujerumani.
Tahasisi za kimataifa zinazoshughulika na utamaduni wa kimataifa kuanzia
mwaka jana zilianza mkakati kutafuta bendi ya kiafrika inayolitangaza bara
la Afrika kwa kutumia muziki, na kuweka utaratibu wa kuzipigia kura bendi
hizo katika tovuti mbali mbali online na offline,Ngoma Africa Band ikajichulia
ushindi wa mamlioni ya kura, pia imegundulia kuwa bendi hiyi inakubalika na
 mamilioni  ya washabiki wa mataifa mbali mbali, 
Mzimu huo wa muziki kutoka Bongo unadaiwa kuwa na wafuasi milioni
50 duniani kote,hali hii inatishia maporomota wa muziki wa kimataifa,
kuwa FFU ni mali ya mamilioni ya washabiki,ni bendi ambayo kipenzi
cha mamilioni ya washabiki. katika kambi yao hii www.ngoma-africa.com
inakadiliwa kuwa na mamilioni ya lank.
Tunawatakia kila yaliyo mema vichaa wetu

Monday, July 9, 2012

BET Awards 2012 Jay-Z, Beyoncé, Kanye West and Kim Kardashian.

Sitting front and center, music’s hottest couples made their presence known at the BET Awards 2012. Jay-Z, Beyoncé, Kanye West and Kim Kardashian were spotted throughout the night enjoying performances by stars like Nicki Minaj, Usher and gospel singers Jessica Reedy, Y’anna Crawley, Amber Bullock and Yolanda Adams.

After standing to congratulate Kanye on his win, Kim watched eagerly as Jay and 'Ye accepted the BET Award for Best Group.

During their speech, Yeezy thanked fellow rap labels Young Money and MMG for boosting his music-making ambitions and gave a special nod to rapper Big Sean for winning the award for Best New Artist.

Madea's Witness Protection.


Box Office: Ted, Magic Mike Edge Out Madea

Seth MacFarlane's comedy had best opening ever for R-rated film.


Madea Gets Edged Out By Ted, Magic Mike
It was raining men — and teddy bears — at this weekend's box office. And the numbers surprised even the most optimistic observers.

Family Guy creator Seth MacFarlane's first feature film venture Ted smashed records with a $54.1 million take and the No. 1 crown: the best performance in history for an R-rated comedy. The Mark Wahlberg starrer (his co-star is a human-like teddy bear) easily beat the other new entries this weekend, Magic Mike and Madea's Witness Protection.

But Mike had plently of dollar bills stuffed into its G-string, to the tune of $39.2 million and way better than expected (unless you ask anyone interested in seeing Channing Tatum's bare chest) for an R-rated film.

Coming in third place was Tyler Perry in Madea's Witness Protection. Though the film couldn't compete with talking bears and shirtless men, it did pull in an impressive $26.4 million.

On the indie film end of the spectrum, Sundance winner Beasts of the Southern Wild opened to strong numbers in four theaters in New York and Los Angeles, and is expected to roll out to other cities in the coming weeks.

Next week, The Amazing Spider-Man goes head-to-head with Oliver Stone's Savages for the most Fourth of July box office fireworks.

Morgan Freeman Says U.S. Still Has No Black Presiden



The Oscar winner says Barack Obama’s white “mama” only makes him mixed race.



Morgan Freeman’s latest comments in defense of President Barack Obama against his opponents will likely be overshadowed by his controversial take on Obama’s racial identity — it’s definitely a feather ruffler.

While talking to NPR about his latest movie, The Magic of Belle Isle, the conversation turned to politics and the President's critics. That's when the actor said he thought Obama should not be called America’s first Black president.

“First thing that pops into my head regarding our president is that all of the people who are setting up this barrier…they just conveniently forget that Barack had a mama, and she was white — very white American, Kansas, middle of America,” Freeman told NPR. “There was no argument about who he is or what he is. America’s first Black president hasn’t arisen yet. He’s not America’s first Black president — he’s America’s mixed-race president.”

In the interview, The Dark Knight Rises star goes on to say that he has been disappointed by the Republican Party and Obama opponents' unfair treatment of the President. But Freeman's comments about the Obama's level of Blackness — which will certainly be viewed as offensive by many — opens a Pandora's box discussion on race. Like, when did being biracial not make you Black? Shouldn’t it be a biracial person’s choice to choose how he or she is identified? And can there ever be an all-“Black” president in this country given America’s race mixing history due to slavery?

Maybe one day Freeman will elaborate more fully on this topic. In the meantime, comments by website and blog commenters should definitely fill the void.

Usher step - son has declare brain dead



UPDATE: Kyle Glover, son of Tameka Foster and stepson of Usher, has been declared brain dead by doctors at an Atlanta children's hospital, TMZ reports. The 11-year-old was airlifted there after being hit by a jet ski in Lake Lanier, and has not experienced any brain activity since.

Usher arrived at the hospital late last night to join his estranged wife Tameka, who hasn't left the critical care unit since she arrived yesterday afternoon.

No decision has been made as to whether or not to take Kyle off of life support.

PREVIOUS: Kyle Glover, the 11-year-old son of Usher's estranged wife Tameka Foster, has been rushed to an Atlanta hospital following a jet ski accident today, TMZ reports. He's in currently in critical condition.

According to sources, Glover was struck by a jet ski while lounging in an inner tube on Lake Lanier and hit in the head. He was unresponsive when taken out of the water and remained that way when he reached the hospital.

TMZ reports that Usher chartered a plane for his ex, who was out of town, so she could rush to her son's bedside. Despite their ongoing divorce drama, sources say Tameka is extremely grateful to Usher for the gesture and is currently at the hospital anxiously awaiting further news about Glover's condition.

Prayers go out to Kyle Glover and his family for a quick recovery.